-->

TANZIA : Aliyekuwa Mume wa Irene Uwoya afariki dunia

Aliyekuwa Mume wa zamani wa Muigizaji Irene Uwoya na Mchezaji wa Burundi, Hamadi Ndikumana Katauti amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.

Siku ya Harusi ya Irene Uwoya aka Oprah na Ndikumana Hamad ‘Katauti’

Taarifa za kifo cha Ndikumana zimethibitishwa na Muigizaji Irene Uwoya ambaye alikuwa mke wake wa ndoa na kufanikiwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Baaada ya muda EATV ilifanikiwa kumpata Haruna Niyonzima ambaye ni moja ya watu wake wa karibu, na kusema kwamba chanzo cha kifo cha Ndikumana ni maumivu ya kichwa aliyoyapata ghafla alipotoka mazoezini jana jioni.

Ndikumana na Uwoya walifunga ndoa Julai 2009 jijini Dar es salaam katika kanisa la Mt. Joseph, na walitengana baada ya  muda mfupi.

eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364