-->

Viongozi, Wasanii Pamoja na Wadau Wamlilia Samweli Sitta

Viongozi, wasanii pamoja na wadau mbali mbali nchini wamlilia aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samweli Sitta aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo wakati akipatiwa matibabu nchini Ujerumani.

samweli-sita

Viongozi hao pamoja na wadau wameandika ujumbe mbalimbali katika mitandao ya kijamii kuonyesha kuwa taifa limepoteza mtu muhimu.


Makonda

Asante baba umenifundisha uongozi,Siku zote umeniambia nianze na mambo magumu kwanza ndiyo nifanye mambo mepesi,niwe na ngozi ngumu na wala nisikate tamaa. Hukuacha kuniombea na kunitia moyo hata wakati unaumwa, hakika wewe ni mwalimu ambae alama zako hazitafutika kamwe maishani mwangu.

Umenisomesha na hata kuniozesha, niseme nini ili dunia ielewe kuwa kwangu ulikuwa zawadi kutoka kwa Mungu,unyenyekevu,upole, na ujasiri wako ni dira tosha ya kuwatumikia Watanzania ambao mpaka sasa nina uhakika unawaombea. Nenda Mzee Sitta acha niendeleze viwango na kasi kwani ndiyo urithi ulioniachia.

Mwigulu Nchemba
Umenifundisha,umeniongoza kwenye siasa na kazi za serikali.Hakika tumepoteza mzazi,mlezi na kiongozi wa mfano.Pumzika kwa amani Mzee wetu Samwel Sitta.

Mrisho Mpoto

Pumzika kwa Amani baba yangu mzee Sita mbele yako nyuma yetu, pole nyingi kwa familia yote ya mzee #Sita pole Rafiki yangu @paulmakonda najua msiba Mkubwa sana kwako.

Mohamed Dewji
Pumzika kwa amani Mzee Samuel Sitta. Mungu ailaze roho yako mahala pema peponi. Tutakukumbuka kwa upendo na uzalendo kwa wananchi wote wa Tanzania.

Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini (TAFF)Mwakifamba Simon
“Rest in peace samwel sitta umeondoka kimwili kifikra bado unaishi nasi kwa busara na hekima ulizokuwa umejaaliwa.

Shamsa Ford
‘Mungu aipumzishe roho yako mahali pema peponi baba yetu.

Diamond Platnumz
“May God Rest your Loyal and Humble Soul in Peace,”

JB
“Pumzika kwa amani Mzee Sitta..”

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364