-->

Ali Kiba: Serikali Iweke Mkono Bongo Movie

MWANAMUZIKI Ali Saleh Kiba amesema ingekuwa jambo zuri kama wasanii wa Bongo Movie watapewa nguvu zaidi na serikali.

lulu325
Kiba ameyasema hayo wakati akizungumzia ushindi wa Watanzania Single Mtambalike ‘Rich Rich’ na Elizabeth Michael ‘Lulu’ wakati wa tuzo za African Magic People’s Choice Awards zilizofanyika katika Hoteli ya Eko kwenye Kisiwa cha Victoria jijini Lagos, Nigeria, usiku wa kuamkia jana.
Akizungumza mjini hapa, Kiba alisema kuna mengi yanawezekana lakini lazima kuwe na nguvu ya serikali kama sehemu ya kuunga mkono.
Kiba ambaye alitumbuiza katika tamasha hilo, aliungana na Rich na Lulu kusherehekea ushindi wao wa tuzo hizo kubwa zaidi katika filamu barani Afrika.

Chanzo: GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364