-->

Chilo Afungukia Kupotea Tamthilia za Nyumbani

Msanii wa filamu, Mzee Chilo amedai wamiliki wa runinga nchini ndio waliosababisha kupotea kwa tamthilia za nyumbani kwa kuzikwepa na kuonesha za kigeni.

aaa

Muigizaji huyo ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya Pilipili Entertainment, ameiambia Bongo5 kuwa hali hiyo imesababisha wazalishaji wa filamu nchini kukaa na kazi zao ndani bila kuwa na sehemu za kuzipeleka.

“Kilichopoteza tamthilia zetu ni runinga zetu, wakawa wanaamua kuonesha tamthilia za kigeni sijui kwao ndio zilikuwa rahisi?” amesema Chilo.

“Lakini sasa hivi naona wameanza kurudi na kutuona sisi ni wa muhimu, wanajali kazi zetu. Hii italeta makubwa katika tasnia yetu kwa sababu wasanii wanajengwa na tamthilia, hao wote wanaotajwa akina Ray, Kanumba na wengine wametokana na tamthilia kwa sababu tamthilia unaangalia nyumbani kwako na familia yako,” ameongeza.

Pia Mzee Chilo amesema baada ya kupata serikali inayowasikiliza wananchi wake ana imani kila kitu kitaenda sawa mwaka 2016.

Chanzo: Bongo5

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364