-->

Davina: Nimezaa Sijazeeka na Bado Nalipa

Staa wa Filamu za Kibongo, Halima Yahya ‘Davina’ amedai kuwa kuzaa siyo kuzeeka kama wasanii wengine wanavyodhani bali ni kupata heshima na kupendeza kama alivyonawiri yeye.

Davina

Davina

Akizungumza na Ijumaa, Davina alisema kuwa yeye ni mama wa watoto lakini kila kukicha anazidi kupendeza na kuonekana ‘kigori’ tofauti na watu wanavyodhani.

“Unajua kuna baadhi ya watu wanadiriki hata kutoa mimba kwa sababu tu wasizeeke kwa kuzaa lakini wanaikosa furaha ya kuitwa mama, mimi napendeza kwa sababu sina stress, watoto wangu ndiyo kila kitu,” alisema Davina.

Chanzo: GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364