-->

Dayna Nyange Amuonea Wivu Roma

MWANADADA anayefanya poa kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Mwanaisha Nyange ‘Dayna Nyange’ hivi karibuni amedai kuwa anamuona wivu staa wa Hip Hop, Roma Mkatoriki kutokana na hatua aliyoifikia ya kufunga ndoa Jumamosi iliyopita mkoani Tanga na mchumba wake wa muda mrefu.

Dayna-nyange3

Dayna anasema amekuwa mtu wa karibu wa Roma kwa muda mrefu sasa ambapo amewafahamu wapendanao hao tangu mwaka 2008 na anashukuru kuona wametimiza ahadi yao ya kuoana lakini kwake pia hiyo ni changamoto ya kuhakikisha pia anaingia kwenye ndoa.

“Roma amefanya kitu cha msingi, ninamuonea wivu kuingia kwenye maisha ya ndoa na ninafikiri amenikumbusha pia kutakiwa kulitimiza hilo jukumu,” alisema Dayna. Nyange.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364