-->

Hii Ndiyo Idadi ya Filamu Zilizokamatwa na Bodi ya Filamu Hadi Sasa

Katika hatua za kupamba na kazi za filamu ambazo zinaingizwa nchini kinyume na sheria na kuikosesha serikali mapato, Bodi ya Filamu tayari imekamata zaidi ya kazi za filamu 656,000 ambazo zimeingizwa nchini kinyume na sheria.

bodi ya filamu32

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisoo

Akizungumza na Bongo5 Jumatano hii, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisoo alisema wao kama bodi ya filamu bado wanapambana na watu hao ambao wanaikosesha serikali mapato.

“Mpaka sasa hivi tumekamata kazi 656,000 na bado msako unaendelea,” alisema Joyce. “Sisi tunafanya huo msako lakini pia Wananchi wanatakiwa kutoa taarifa za watu kama wao ili kurahisisha namna ya kuwakamata,”

Katika hatua nyingine Joyce amewataka wasanii kupeleka kazi zao bodi ya filamu ili zikaguliwe kabla hazijaingia sokoni kuepuka kuingiza sokoni kazi ambazo hazina tija kwa Watanzania.

Bongo 5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364