-->

JB Aanza Kushoot Tamthilia Yake Mpya ‘Kiu ya Kisasi’

Msanii mkongwe wa filamu na mtayarishaji, Jacob Stephen ‘JB’ amewataka mashabiki wa kazi zake za filamu kukaa mkao wa kula kwa ujio wa tamthilia yake mpya iitwayo ‘Kiu ya Kisasi’.

JB90

Kupitia instagram, JB ameandika:

Wapenzi wa Jerusalem nilikuwa sijawapa habari ya kazi tunayoendelea nayo sio filamu bali ni tamthilia. Inaitwa Kiu ya Kisasi. Ningependa wapenzi wangu wote muione kazi hii. Tatizo ni runinga gani mko wengi. Tayari tumeanza mazungumzo na runinga nyingi zilizoonyesha nia ya kuirusha lakini tutaangali wapi tutalipwa vizuri, na wapi wapenzi wetu mko wengi…nawapenda.

Katika post nyingine aliandika:

Ratiba yetu wapenzi wa Jerusalem Films tunaendelea kuchukua picha za tamthilia yetu ya Kiu ya Kisasi hadi mwezi tano. Lakini mwezi huo wa tano tuta achia filamu ya ‘Kalambati Lobo’ ambapo tumecheza mimi JB na Diana Kimaro. Kisha itakuja Chale Mvuvi, amecheza Shamsa Ford na Haji Adam, halafu mwezi wa tano nitaingia tena kazini kufanya ile movie yangu na King Majuto….nawapenda.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364