-->

Jinsi Ya Kutambua Simu Feki

1. Kabla hujanunua simu mpya hakikisha unaandika namba hii *#06#, kwenye simu hiyo au ambayo tayari umenunua.
2. Ukishaandika itaonyesha namba ya pekee (serial number) au IMEI (International Mobile Equipment Identity) ambayo ni lazima ziwe tarakimu 15 au zaidi na ni lazima ianze na 35.
3. Angalia kwa makini kama namba unazoziona zinafanana moja kwa moja na namba zilizoandikwa katika simu yako kwenye sehemu ambayo betri inakaa. Namba hizi zinapaswa kufanana kwa simu ambayo ni halisi. Kama hazifananani simu hiyo ni feki.
4. Tuma namba ya pekee (IMEI) kwenda namba 15090 na utapokea ujumbe mfupi unaoelezea kama simu yako ni orijino au feki.

simu

KUJUA UBORA WA SIMU
1. Katika namba hizo namba ya sasa (7) na ya nane (8) ndizo zinazohakikisha ubora wa simu yako.
2. Kama namba ya saba na ya nane ni 00 ina maana kuwa simu yako imetengenezwa kwa ubora wa juu kabisa katika viwanda vya kuaminika.
3. Kama namba ya saba na ya nane ni 01 au 10 ina maana simu yako imetengenezwa Finland na ina ubora wa juu pia.
4. Kama namba ya saba na ya nane ni 13 ina maana simu yako imeunganishwa katika nchi za Azerbaijan na ni hatari kwa matumizi ya afya yako.
5. Kama namba ya saba na ya nane ni 02 au 20 ina maana simu yako imeunganishwa katika nchi ya Emirates na ina kiwango cha chini, lakini siyo feki.
6. Kana namba ya saba na ya nane ni kati ya 03 au 30 au 04 au 40 ina maana simu yako imentengenezwa China, lakini ina ubora mzuri ila haijafikia zile zenye 00, 01 au 10.
7. Kama namba yako ya saba na ya nane ni 05 au 50 ina maana simu yako imetengenezwa labda Brazil au USA ama Finland.
8. Kama namba ya saba na ya nane ni 06 au 60, simu yako imetengenezwa Hong Kong, China au Mexico.
9. Kama namba ya saba na ya nane ni 08 au 80, simu yako imetengenezwa Ujerumani na ina ubora wa kawaida.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364