-->

KR Mullah Afunguka Kuhusu TMK Family na Rada Entertainment ya TID

Rappa KR Mullah amesema yeye bado ni msanii wa TMK Wanaume Family na Radar Entertainment yupo kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali kutoka kwa vijana.

Muimbaji wa Bongo Fleva TID akiwa na rapper KR Mullah

Muimbaji wa Bongo Fleva TID akiwa na rapper KR Mullah

Akiongeza na Bongo5 Jumapili hii, KR amesema hawezi kuondoka TKM Wanaume Family kwa kuwa yeye ni mmoja kati ya waanzilishi wa kundi hilo lenye maskani yake Temeke jijini Dar es salaam.

“Mimi sijaondoa Wanaume Family, bado nipo kule sema lazima ujichanganye kidogo na wasanii ili kubadili ladha ya muziki, Rada kuna vijana wengi wapya na kukaa nao kunanipa vitu fulani ambavyo vinaweza kuboresha muziki wangu,” alisema KR.

Pia KR alisema yeye ni mmoja kati ya waanzilishi wa Kundi la TMK Wanaume Family hivyo hawezi kulitosa kundi hilo.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364