-->

Kusaka Mpenzi Kwenye Simu, Sitosahau – Linah

Msanii wa Bongo fleva Linah a.k.a ndege mnana amefunguka moja kati ya vitu ambavyo hawezi visahau katika maisha yake yote.

Linah Sanga8

Akizungumza na Enewz Linna alisema kwamba moja ya kitu hicho ni tukio ambalo walilifanya yeye na mwenzie kipindi wanasoma kwani walikuwa wana tabia ya kujaribu kupiga namba tofauti tofauti ili kutafuta mpenzi.

“Nilifanikiwa kumpata mwanaume ambae nikawa ninawasiliana nae lakini siku tunaenda kuonana nae tulikutana na kitu hicho ambacho siwezi kusahau maana tulikutana na mtu ambae hatukutegemea kutokana na sauti yake ambavyo tulikuwa tukiisikia katika simu tukaamua kutojitokeza “,alisema Linna.

eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364