-->

Msanii wa Nigeria awatamani Ali Kiba, Diamond

MSANII wa muziki wa pop kutoka nchini Nigeria, Omo Alhaji Ycee, ametoa msaada wa Sh milioni moja katika kituo cha wanajamii cha Kigamboni Community Center (KCC) ili zisaidie kutokomeza umasikini.

Omo-Alhaji-Ycee

Omo Alhaji Ycee

Msanii huyo ambaye yupo katika ziara ya kutangaza muziki wake, aliliambia MTANZANIA kwamba ameamua  kuunga mkono kituo hicho kwa sababu  ya kujitolea  kwao kukuza vipaji na kuendeleza elimu kwa jamii.

Katika hatua nyingine, msanii huyo amedai atafanya mazungumzo na wasanii wanaofanya vizuri nchini katika muziki ili afanye wimbo wa kushirikiana.

“Wasanii ninaotamani kufanya nao wimbo ni Ali kiba na Diamond kwa kuwa wapo katika kiwango cha kimataifa,” alisema Ycee ambaye baada ya kumaliza ziara yake hapa nchini ataelekea nchini Afrika Kusini.

Mtanzania

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364