-->

Najma: Sijali ‘Makombo’ kwa Baraka

Mwanamuziki Najma Dattan ‘Naj’ ameibuka na kusema kuwa kwa msanii mwenzake Baraka Da Prince amefika wala hajali ametoka na wanawake wangapi kwa sababu hata yeye ana ‘pasti’ yake.

BARAKA78

Akizungumza na Ijumaa, Najma alisema kuwa amekuwa akiwashangaa wasichana waliopita kwa Baraka ndiyo wanamuongelea kila siku wakidai anakula makombo lakini Baraka mwenyewe haongelei kabisa uhusiano wa watu wake wa zamani.

“Sijali ametoka na wangapi, hayo ni maisha ambayo kila mtu anapitia. Niseme tu kwamba sijawahi kumtambulisha mwanaume kwetu, hapa kwa Baraka nahisi nimefika kwa sababu ndiye mwenye penzi la kweli, kitakachofuata muda si mrefu ni ndoa tu kwani wazazi wetu wanaujua uhusiano wetu,” alisema Najma.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364