-->

Riyama: Mtuache Tulale!

STAA wa filamu za Kibongo, Riyama Ally amewafunga midomo wote waliokuwa wakibeza uhusiano wake na msanii chipukizi wa muziki wa Bongo Fleva, Haji Mwalimu Mzee ‘Leo Mysterio’, baada ya kufunga naye ndoa hivi karibuni.

RIYAMA13

Minong’ono ilikuwa mingi mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kuwa Riyama yupo kwenye uhusiano na Serengeti Boy kwa vile kijana huyo ni mdogo wake kiumri kwa miaka saba zaidi.

Akiondoa utata, Riyama alisema wanaojua kusugua midomo waendelee lakini wao tayari wameshakuwa mwili mmoja, yeye akiwa mali halali ya Leo Mysterio.

“Wamesema sana, lakini sasa limewashuka shuuu! Wengine walisema sijui tunatafuta kiki, mara ooh! Sijui nimemzidi umri… inawahusu nini? Tayari tumeshafunga ndoa, sasa watuache tulale. Kama vilimilimi tushawakata,” anasema Riyama.

Mysterio ana umri wa miaka 26 huku Riyama akiwa na miaka 33, miaka saba zaidi ya mume wake huyo anayetamba kupendana mpaka kifo kitakapowatenganisha.

Riyama anasema: “Mimi najiheshimu sana, ndiyo maana huwezi kunikuta kwenye skendo yoyote. Hata mavazi yangu siku zote huwa ya heshima. Najitambua sana.

“Sasa kama kupenda au kupendwa na mtu mliyezidiana umri ni skendo, nipo tayari kwa hiyo. Mimi nilichoangalia ni mapenzi ya kweli, siyo umri. Mume wangu tumeelewana na naona kila mmoja anakidhi haja za mwenzake, sasa tatizo nini?

“Nampenda na nitamheshimu mume wangu hadi kifo kitakapotutenganisha, wanaosema na waseme, sisi tumeziba masikio yetu. Wala hatufikirii kuachana. Sisi ni wa maisha.

Mtanzania

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364