-->

Rose Ndauka: Wanaume Wakware Bado Wananisumbua

STAA wa filamu nchini, Rose Ndauka, ameweka wazi kwamba licha ya kujibidisha kwenye ubunifu wa kazi mbalimbali za kumwingizia kipato anazozifanya, hujikuta akikutana na idadi kubwa ya wanaume wakware wanaomtaka kimapenzi badala ya kufanya naye biashara.

Rose Ndauka

Ndauka ambaye kwa sasa anajishughulisha na ujasiriamali, alisema amekua akibuni njia mbalimbali za kumwingizia kipato ili aendane na hali halisi ya maisha kwa sasa lakini wanaume wakware humkwamisha kwa usumbufu juu yake.

“Kila kazi ina changamoto zake, sikatai wanaume lakini wengi wao huja kunitaka kimapenzi, badala ya kuzungumzia masuala mengine ya biashara, nachukizwa sana na wanaume wa aina hii,” alieleza Ndauka.

Mtanzania

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364