-->

Shilole Amtesa Nuh kwa Tatuu

Shilole-na-Nuh-Mziwanda-600x400

Kama huna taarifa basi kaa ukijua kuwa, lile penzi lililokuwa na sarakasi nyingi, mara wafumaniane, mara wapigane, mara waachane sasa limefikia mwisho kama siyo kikomo. Nawazungumzia mastaa wawili, Nuh Mziwanda na Shilole ambao wametangaza rasmi kwamba kila mmoja kuwa na hamsini zake.

Shilole amesema kuwa, haoni sababu ya kuendelea na Nuh kwa kuwa anahisi anambana tu na wala haoni faida kubwa ya kuwa naye.

Kufuatia maneno hayo, Nuh ameona isiwe kesi, amekubali yaishe lakini taarifa iliyotua kwenye ukurasa huu ni kwamba, jamaa anahaha kufuta tatuu aliyojichora mwilini mwake yenye jina la Shilole.

“Kimsingi ile tatuu ya Shilole inamtesa sana Nuh,” alisema rafiki wa msanii huyo.
Nuh anasemaje? Msikie: “Ni kweli ila hii tatuu nitaifuta nitakapompata wa kuziba pengo la Shilole.”

Chanzo:GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364