-->

Shilole Atoboa Kilichomsukuma Kupatana na Nuh Mziwanda

Baada ya hivi karibuni Sholole na Nuh Mziwanda kupatana, Shilole amefunguka na kuzungumzia nini kimemsukuma mpaka akapatana na mkali huyo wa wimbo ‘Jike Shupa’.

SHILOLE77

Wawili hao ambao walikuwa wapenzi waliachana kwa kutupiana maneno huku Nuh Mziwanda akionekana kumlaumu Shilole kwa kumpotezea muda.

Akiongea na Uhead ya Clouds FM Ijumaa hii, Shilole amedai ameamua kumaliza tofauti zake na Nuh Mziwanda kwa kuwa muimbaji huyo wa ‘Jike Shupa’ alikuwa anapoteza kujiamini pale anapokutana naye.

“Nikwambia kitu situation moja ambayo ipo, Nuh akiniona mimi huwa anapoteza kujiamini,” alisema Shilole. “Sasa ili kumueka sawa na aweze kuwa vizuri lazima na mimi nimwonesha am good. Kwa hiyo alivyoniona nipo good na yeye akawa fresh na furaha imerudi na nazani maisha yanaendelea,”

Hata hivyo mkali huyo wa wimbo ‘Say My Name’ alikanusha kurudiana na Nuh Mziwanda huku akidai kwa sasa wao ni washkaji.

Bongo5

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364