-->

Sholo Mwamba ni Mfa Maji”- Man Fongo”

Image result for sholo mwamba na  mani fongo

Msanii wa miondoko ya singeli Man Fongo amesema hawezi kukaa na kumzungumzia Sholo Mwamba kwa madai yeye ni mfa maji ndiyo maana haishi kutapa tapa kila uchao kumtaja.

Man Fongo ameeleza hayo baada ya masaa machache kupita tokea kuonekana kwa ‘video’ ya Sholo iliyorushwa na EATV katika kipindi cha ‘FRIDAY NIGHT LIVE’ (FNL) usiku wa kuamkia leo, ikiwa imemuonyesha akimlaumu msanii mwenzake kuwa hana kipaji cha kuendelea kufanya muziki mzuri ndani ya mwaka 2018 huku akimtaka arejee katika fani yake ya awali ya ‘DJ’.

“Mimi kwa sasa siwezi kumzungumzia mtu yeyote kwa maana naangalia muziki wangu kwa sababu ndiyo unaonifanya nieleweke kwa wadau wangu, pia unasababisha familia yangu ipate kula. Kwa hiyo mtu akitaka kutoka kwa kutumia kiki na kupitia mgongo wangu nakuwa bado simuelewi. Hivyo siwezi kumtumikia Sholo Mwamba ‘eti aniambie mimi nirudi katika fani yangu ya ‘DJ’ wakati yeye hayupo katika ‘manegement’ yangu na yeye ni msanii kama mimi”, alisema Man Fongo wakati alipofanyiwa mahojiano maalum.

Pamoja na hayo, Man Fongo ameendelea kwa kusema “ninachopenda kumshauri Sholo Mwamba ni kwamba atoe ngoma mpya ili aweze kusikilizwa na raia anachokifanya, apambanie muziki wake aweze kufika mbali na asiangalie muziki wangu mimi”, alisisitiza Man Fongo.

Kwa upande mwingine Man Fongo amesema mwaka 2018 amejiandaa vizuri katika ufanyaji kazi wake na wala haiwezi kuwa kama alivyosema mpinzani wake huyo ambae kwa muda mrefu wamekuwa wakitoleana mapovu katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

“Kazi mpya nimeangusha juzi tu na mpaka sasa ninapo kwambia inafanya vizuri hivyo Sholo Mwamba ni mfa maji tu kama mtu ambae anatapa tapa yaani mfa maji haishi kutapa tapa. Kwa hiyo ameona bora apate kiki kwa mgongo wangu ili aweze kutoka”, alisema Man Fongo.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364