-->

Sina Tatizo na Hakeem 5 – Ali Kiba

Msanii Alikiba ametolea ufafanuzi tuhuma zilizotolewa na msanii mwenzake hakeem 5, huku akisema hataki hata kumuona kwani si mtu mzuri na amekataa kufanya naye colabo.

ALI KIBA54

Ali Kiba ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na east africa Radio, na kusema kwamba yeye binafsi hana tatizo na Hakeem 5, kwani yeye ni kama ndugu yake, na hata deni lake la kolaboalishalipa, kwani alishafanya naye kazi kabla hajachukua likizo ya kufanya muziki.

“Hakeem ni ndugu yangu na ataendelea kuwa ndugu katika dunia sikumtendea mabaya, lakini hakuelewa vitu gani vinatakiwa viendelee sasa hivi, deni ambalo anasema ananidai nililipa nikamfanyia nyimbo safi sana ndio nikachukua ile likizo ya kufanya muziki kwa miaka mitatu, baada ya likizo nikawa natangaza kurudi nikarudi vizuri, baada ya kurudi Hakeem anataka tufanye video, mi nili-understand, lakini production ndio tuliposhindwana”, alismea Ali Kiba.

Alikiba aliendela kuwa baada ya hapo kuna siku walikutana studio, na Hakeem alimtaka tena Alikiba wafanye colabo, lakini Alikiba alishindwa kufanya kolabo hiyo kutokana na mkataba aliokuwa nao kwa wakati huo hakutakiwa kufanya kolabo yoyote, na ndipo alipochukia kwa kutoelewa.

“Nikakutana nae studio akawa anataka tufanye featuring, na kwa kipindi hicho na mimi mkataba wangu sikutakiwa kufanya colabo, huwezi kuvunja mkataba, sasa Hakeem hajanielewa”, alisema Alikiba.

EATV.TV

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364