-->

Tausi Mdegela Kuolewa Mke wa Pili

Msanii wa filamu wa Tanzania mwenye muonekano wa kipekee na kipenzi cha watoto, Tausi Mdegela, ameutaarifu umma kuwa anatarajia kuolewa kuwa mke halali wa mpenzi wake wa siku nyingi ambaye ni msanii wa muziki wa taarabu, Prince Amigo.

Tausi akiwa na mpenzi wake Prince Amigo

Akizungumza na mwandishi wa EATV, Tausi amesema suala la ndoa ni mipango lakini ni jambo ambalo lipo, kwani tayari wamekuwa kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mpenzi wake huyo ambaye ni mwanamuziki wa taarab, ambaye tayari ana mke wa kwanza.

“Ndoa ni mipango mtuombee Mungu tufike mbali, ni muda mrefu tumeanza tunaishi pamoja, ila Amigo ana mke mkubwa, kwa hiyo mimi nasubiria kuwa mke mdogo, hapa akiongezeka watatu ndio itakuwa mtihani, wawili tushatosha wengi wa nini, hapo ndo tutapigana sasa, na tukigundua kuna wa tatu hapo ndio litakuwa lingine, na mke mkubwa kashakubali”, amesema Tausi.

Tausi ameendelea kwa kusema kwamba yeye hajali maneno ya watu wanayosema kuhusu mahusiano yake hayo, kwani anachoangalia ni maisha yake na sio watu wanasema nini.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364