-->

Thea:Tunatetea Haki Yetu

MSANII wa filamu za Kibongo, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ ameibuka na kuwabeza watu wanaowaponda waigizaji kwa kitendo chao cha kuandamana kupinga uuzwaji holela wa sinema za nje kwa kuwaambia waendelee kutukana kwani wao walifanya hivyo ili kutetea haki yao.

Akipiga stori na Za Motomoto News, Thea alisema wao walifanya hivyo kwa kuona inafaa, sasa kama kuna watu wengine wanatoa maneno machafu juu yao watakuwa na lao jambo kwa sababu hata Hollywood ilifi ka kipindi tasnia ikasimama kabisa.

“Ninachoweza kusema ni tumuombe Mungu hekima yake ituangalie, tujitathmini pale tulipoanguka tuparekebishe, wanaotukana waendelee kutukana lakini mimi fi lamu ndiyo inayoniweka mjini, nakula, nalala na kuvaa kwa kazi hiyo,” alisema Thea.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364