Ukimya wa Odama Wawapa Jibu Mastaa!
Staa wa sinema za Kibongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka kuwa ukimya wake wa muda mrefu umewapa jibu mastaa wenzake kwani kuibuka kwake na sinema mpya kumezua gumzo na kumpa heshima ya kuendelea kusimama kama msanii.
Odama ameliambia Wikienda, kuwa alipoamua kukaa kimya alikuwa na sababu kwani alikuwa ametuliza kichwa kuhakikisha anaibuka na sinema itakayozidi kumjengea heshima kwa mashabiki wake.
“Nimeibuka na Mkwe, filamu hiyo imenifanya nijisikie mwenye heshima sana hata kutoka kwa mastaa wenzangu,” alisema Odama aliyewahi kutamba na Sinema kama Jada, Figo, Family War na nyinginezo.
Chanzo:GPL