-->

WCB Wadaiwa Kupora Wimbo wa ‘Bado’

Producer Frag kutoka Uptown Music ametumbua jipu baada ya kuibuka na kusema kuwa yeye ndiye aliyetengeneza wimbo wa Bado wa Harmonize na Diamond.

Fraga1

Producer kutoka Uptown Musi Fraga

Frag aliiambia Enewz kuwa pamoja na kazi kubwa aliyoifanya kuhakikisha ngoma hiyo inakuwa poa lakini bado WCB wakamzima na hawakumlipa hata senti tano na kuambulia elfu thelathini pekee ya nauli.

“Kawaida nikifanya kazi uptown music lazima saini zangu ziwepo lakini kwa kule wasafi saini zangu hazikuwekwa, na sijajua kwasababu gani hazikuwekwa wangeweka tu ata ile saini ya jina langu ili kunitengezea heshima kwa watu wengine ”, alisema Frag.

Eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364