-->

Wema Sepetu Atumia Show ya Vigoma Tanga Kuzindua Bidhaa Yake Mpya

Malkia wa filamu Wema Sepetu ametumia show yake ya vigoma iliyofanyika Jumamosi hii katika Viwanja vya Mkwakwani mkoani Tanga kuzindua bidhaa yake mpya ya viatu vya kike.

wema-sepetu-2

Mwigizaji huyo ambaye mwishoni mwa mwaka jana alizindua bidhaa yake ya kwanza ya lipstick, amesema bidhaa hiyo itaanza kupatika madukani hivi karibuni.

“Wakati naanza kutumia jina langu kwa ajili ya kuendeleza brand yangu ya Wema Sepetu, nilianza na lipstick na sasa nimekuja na viatu vya kike,” alisema Wema mbele ya umati wa watu waliojitokeza katika usiku wa vigoma. “Hivi viatu ni vya kitamaduni kabisa kwa sababu wanasema uzalendo kwanza,”

Aliongeza, “Kwa hiyo nilisema nifanye kitu gani ambacho kitawakilisha na uzinduzi wa hivi viatu, nikasema niandae show ya usiku wa kitu fulani, kwa hiyo nilivyokuwa nataka kuzindua hivi vitu nikasema nitumie akili, nifanye usiku wa Kiswahili, kwa sababu hata hivi viatu vinaenda Kiswahili, nikafikiria usiku wa vigoma, tumeanza Dar es salaam na kutaamua tuje Tanga na baadae mikoa mingine,”.

Mwigizaji huyo amesema anaamini akizunguka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania ataweza kupata support kubwa kwenye bidhaa zake pamoja na kazi zake za filamu.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364