-->

Feza na Lulu Wajitosa Kwenye Bifu la Vanessa na Shilole

Msanii wa filamu Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Feza Kessy wamejitosa kwenye bifu la Shilole na Vanessa Mdee ambalo linaendelea katika mitandao ya kijamii.

SHILOLE546

Chanzo cha bifu ya Shilole na Vanessa hakijatambulika, lakini wawili hao toka jana wamekuwa wakirushiana maneno makali na vitisho katika mitandao ya kijamii hali ambayo imewafanya baadhi ya wasanii kuingilia kati sakata hilo la aina yake.

Muigizaji mahiri Elizabeth Michael ‘Lulu’ alikuwa moja kati ya msanii wa kwanza kutupia neno kwenye ugomvi huo kwa namna ya kushangazwa na jinsi watu wanavyosifia uzuri wao kupitia mitandao ya kijamii.

“Hebu nikazane kusoma nianze ligi za kikubwa na dada zangu wenye madegree na ma masters kama ‘Esilovey’ hizi ligi nyingine zinasikitisha,” aliandika Lulu kupitia Twetter huku akiongeza post nyingine kwa kuandika “Watu wanashindania uzuri, makalio, followers, nguo, outings, umaarufu, umaarufu wenyewe kama network ya mtandao unaokuwaga mpya, full kukatakata,”

Pia msanii wa muziki na mtangazaji wa Choice Fm, Feza Kezzy baada ya kuona stori inakuwa kubwa katika mitandao ya kijamii, aliandika ya moyoni kuhusu jinsi watu wanavyo shabikia mambo yasiyo na maana na kuacha kushabikia mambo ya msingi.

“Yaani watu wa ajabu sana, inabidi mbadilike. Watu wakifanya mazuri or kazi nzuri hamsemi, hamsupport, lakini umbea comments karibu laki moja dah. It’s very sad, bongo we need to change and support our talents Not tear them apart, Ntawacheka sana mkigundua labda hata ma star hawa hawana beef lol,” aliandika Feza kupitia instagram.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364