-->

Polisi wafukua kaburi la dereva wa bodaboda

Moshi. Mwili wa dereva wa bodaboda, Juma Hamis (26) umefukuliwa na polisi kwa ajili ya uchunguzi kubaini chanzo cha kifo chake.

Hamis aliyekuwa mkazi wa Boma Mbuzi alizikwa katika makaburi ya Pasua mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kufukuliwa kwa mwili huo kunatokana na amri iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi.

Hamis alifariki dunia Julai 28 ikidaiwa ni kutokana na kipigo na kuzikwa Julai 29 katika makaburi ya Pasua.

Mwananchi

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364