-->

Profesa Jay Aeleza Sababu za Ukimya

BAADA ya mashabiki wake wengi kutaka kujua kwa nini yupo kimya kwenye anga la muziki, mkongwe Bongo Fleva ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Morogoro, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ ameibuka na kuwaeleza kinachomsibu.

Mbunge wa jimbo la Mikumi na msanii wa Hip hop , Prof Jay

Akipiga stori na baada ya kuulizwa sababu za kuwa kimya, Profesa Jay alisema bado anaweka mambo ya kifamilia sawa na yakishakuwa vizuri ndipo atakaporejea tena.

“Kuna mambo mengi ya kifamilia yananiweka bize, najitahidi kuyaweka sawa yakikamilika mashabiki wangu watarajie muziki mzuri kutoka kwangu. Niwaombe tu wawe na subira kwani mambo mazuri hayataki haraka,” alisema Profesa Jay.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364