-->

Shilole Hakuwa Mke Mzuri Kwangu – Nuh Mziwanda

SHILOLE34

Nuh ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba wakati yupo kwenye mahusiano na Shilole alishindwa kuonesha undani wake, ambao amekuja kuujua baada ya kuachana na penzi kuisha.

“Baada ya mapenzi kuisha mi nimekuwa adui yake, amehack acount yangu ya instagram najaribu kuwacheki wa kurudisha acount yangu wanashindwa kunirudishia anabana kila sehemu, kuna vitu ananifanyia vidogo vidogo ambavyo nimefanya kugundua kuwa hakuwa mwanamke mzuri kwangu, alikuwa anashindwa kuonesha true colour yake nimekuja kuijua baada ya kuachana naye”, alisema Nuhu.

Pia Nuh Mziwanda amesema iwapo wangeachana kwa amani na Shilole asingelazimika kuifuta tatoo hiyo, kwani ni ukweli usiopingika kwamba amemsaidia katika maisha yake.

“Mi ningeiacha tatoo kama Shishi ningeachana nae poa, kila mtu na maisha yake fresh tukionana tunasalimiana hakuna noma, lakini mwenzangu kwenye interviews anasema, akiitwa kwenye interview anaongea hiki kwamba mimi sina kitu, sijui nashindwa kusurvive nakula magengeni, anaongea vitu vingi ambavyo anajaribu kutoa fan base yangu, angekuwa mtu mzuri baada ya kuachana naye tatoo ningeiacha kwa sababu ningejua bado kabaki kuwa rafiki yangu na ni mtu ambaye alinisaidia”, alisema Nuh.

Pamoja na hayo Nuh amesema yeye binafsi hana chuki na msanii huyo ambaye alikuwa naye kwenye mahusiano, na kwa sasa ana mahusiano mengine ambayo asingependa kuyaweka wazi.

Mimi sina ubaya na Shishi , sina ugomvi naye na wala sitaki kufikiria kuja kuwa na bifu naye, nipo kwenye mahusiano lakini siwezi kuweka wazi mahusiano kwenye mitandao ya kijamii, sababu ni mke wangu yuko kwenye moyo wangu, hayupo instagram wala kwenye mitandao ya kijamii”, alisema Nuh.

Eatv.tv

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364