-->

Thea Adaiwa Kuhongwa Gari

STAA wa filamu Bongo, Salome Urassa ‘Thea’ sasa hivi anasukuma mkoko baada ya kutembea kwenye vumbi kwa muda mrefu lakini pia taarifa zilizo nyuma ya pazia zinadai eti kahongwa na mwanaume.

THEA34
Inadaiwa baada ya Thea kumwagana na Michael Sangu, alijiweka kwa mwanaume mwenye nazo na ndiye aliyempa jeuri ya kumiliki gari hilo aina ya Toyota Passo.

“Thea sasa mambo safi, anatembelea makalio baada ya kuhongwa gari na yule bwana wake wa sasa,” kilidai chanzo hicho.

Baada ya kunyaka ‘ubuyu’ huo, Thea alitafutwa, alipopatikana alisema: “Hili gari sijahongwa na katika maisha yangu sitegemei kuhongwa na mtu yeyote, nimenunua kwa hela yangu ninayopata kwenye muvi.”

Chanzo: GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364