-->

Wanaosema Sina Kazi Wanakosea- Idris Sultan

Mchekeshaji maarufu nchini Idris Sultan amesema kwamba wanaosema hana kazi na anazurura tuu kwenye mitandao ya kijamii wanakosea kwa sababu yeye ni msanii.

IDRISS231

Idris amefunguka hayo alipokuwa akihojiwa na mtangazaji Salama Jabir katika kipindi cha Mkasi Tv Show kinachotushwa na EATV.

”Mimi ni ‘Celebrity’ na kwangu kuwa kwenye mitandao ya kijamii kwangu ni kazi kwa sababu siwezi kufanya ‘interview’ na vyombo vya habari kila siku”-Amesema Idris.

Aidha Msanii huyo pamoja na mambo mengine amefunguka kwamba bado hajaoa na wala hana mtoto.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364