-->

Author Archives: editor

Chipsi Zamponza Baby Madaha, Alizwa na Viba...

Post Image

MWIGIZAJI wa filamu za bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’, amejikuta akishikwa na butwaa baada ya kuporwa pochi yake na vibaka wawili waliokuwa katika pikipiki eneo la Makonde, Kunduchi, jijini Dar es Salaam. Mwigizaji huyo alipatwa na mkasa huo usiku wa juzi, wakati akielekea kununua chipsi karibu na kituo cha daladala cha Makonde. Ghafla pikipiki […]

Read More..

Mzee Majuto: Nataka Nikifa Nizikwe Kama Ste...

Post Image

Wiki hii, Mpaka Home ilifunga safari mpaka mkoani Tanga, nyumbani kwa mchekeshaji maarufu wa siku nyingi,  mzee Amri Athumani (68) ‘Mzee Majuto’ kwa lengo la kuyajua maisha halisi ya mchekeshaji huyu. Mzee Majuto anaishi eneo linaloitwa Donge, mkoani humo ambapo anaishi na familia yake nzima akiwepo mkewe kipenzi; Asha, watoto wake pamoja na wajukuu wake. […]

Read More..

Pichaz: Zari The Boss Lady Afanya ‘Ba...

Post Image

Siku zinayoyoma na mwezi ujao panapo majaliwa, Zari atajifungua mtoto wake wa pili na Diamond. Huyo atakuwa mtoto wake wa tano kwa ujumla. Katika kujiandaa na mapokezi ya mtoto huyo, staa huyo wa Uganda amefanya baby shower nchini Afrika Kusini na kuwashirikisha marafiki zake na watu wa karibu.

Read More..

TUZO za EATV: Kwanini Mastaa Wametoswa?

Post Image

MIONGONI mwa habari zinazobamba kwa sasa katika ulimwengu wa mastaa Bongo ni pamoja na Tuzo za EATV 2016, lakini kinachozunguka zaidi vichwani mwa wadau ni kutoswa kwa baadhi ya mastaa wengi wa filamu na muziki katika kinyang’anyiro hicho. Tuzo hizo ambazo zinatarajiwa kutolewa Desemba 10, mwaka huu katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es […]

Read More..

Kajala Masanja: Afunguka Kuhusu Msamy Baby,...

Post Image

STAA wa Bongo anayetesa kwenye filamu, Kajala Masanja amevunja ukimya na kufunguka kuhusu maneno yanayozagaa mitaani yakimtaja kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa nyakati tofauti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Msamy Baby. Kwa muda mrefu sasa, minong’ono hiyo imekuwa ikizagaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii […]

Read More..

Nikki wa Pili Awaasa Mafisadi, Awakumbusha ...

Post Image

Msanii Nikki wa pili ambaye pia ni mwanazuoni anayetoka kundi la Weusi ambalo linafanya vizuri kwenye muziki wa Hip Hop, amewaasa mafisadi juu ya wanachokifanya, huku akiwaonya kuwa maisha bado yatakuwa yale yale hadi siku ya kifo. Kwenye ukurasa wake wa instagram Nikki wa Pili ameandika ujumbe akiwakumbusha watu wanaopenda kujilimbikizia pesa, kuwa hata uwe […]

Read More..

Mama Diamond Adai Nyumba ya Diamond ya Mada...

Post Image

Mama mzazi wa msanii diamond Platnumz amefunguka na kudai kuwa nyuma ya diamond aliyojenga madeli jijini dar es salaam ni yake na sio ya diamond. Hii nikutokana na ahadi alioiweka diamond mwenyewe kipindi ameanza kuijenga. Zaidi msikie hapa  

Read More..

Ommy Dimpoz Awamwagia Sifa BASATA

Post Image

Msanii wa bongo fleva Ommy Dimpoz amelisifia Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kuwafanyia kazi wasanii ambao wanajishughulisha na kuimba mambo yasiyofaa pamoja na matusi katika nyimbo zao. Akipiga story ndani ya eNewz amesema analipongeza baraza hilo kwa kuwachukulia sheria wasanii ambao wanaimba nyimbo zenye matusi na ambazo hazina maadili na kutengeneza maneno na mijadala isiyo […]

Read More..

Dito Awafagilia Mastaa Waliooa, Afunguka Ku...

Post Image

Msanii wa bongo fleva Dito amesema amekaa na mwanamke wake kwa miaka mitano na wamefanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume lakini bado hawajafanikiwa kufunga ndoa. Akiongea ndani ya eNewz Dito amewapongeza wasanii waliofunga ndoa na kusema wamefanya vizuri kutengeneza familia ambazo baadaye zitawasaidiaa kwa kuendeleza vipaji kupitia watoto wao au kuwa wasimamizi wa muziki wanaoufanya na […]

Read More..

Gabo Auzungumzia Umuhimu wa Tuzo za EATV Aw...

Post Image

Msanii wa filamu anayefanya vizuri na filamu ‘Safari ya Gwalu’ Salim Ahmed ‘Gabo’ amesema tuzo ni kitu muhimu kwa wasanii kwa kuwa ni kipimo ambacho kinapima mafanikio ya msanii husika. Muigizaji huyo ambaye anawania tuzo ya muigizaji bora wa kiume katika tuzo za EATV Award, amesema hatua ya kuongezeka kwa tuzo nchini kunasaidia kukuza sanaa. […]

Read More..

Mzee Chilo Awataka Wasanii wa filamu Kubadi...

Post Image

Nguli wa filamu, Ahmed Olotu maarufu kama ‘Mzee Chilo’ amesema anajua tasnia ya filamu inakumbwa na changamoto nyingi lakini wasanii wa filamu wanatakiwa kubadilisha mbinu za kibiasha ili wanufaike na kazi zao. Akiongea na Bongo5 wiki hii, Chilo amewataka wasanii wa filamu kubadili mtazamo wa kibiashara ili waweze kunufaika na kazi zao. “Mimi nasema tutengeneze […]

Read More..

Man Fongo: BASATA Walitaka Kufungia Hainaga...

Post Image

Msanii wa muziki wa Singeli Man Fongo amesema aliitwa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) na kuhojiwa kuhusu maudhui ya wimbo wake ‘Hainaga Ushemeji’ ambao umeshafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio. Akiongea na Bongo5 wiki hii, Man Fongo amesema aliachiwa na baraza hilo baada ya kuonekana hana hatia. “BASATA walinitafuta wakaniuliza vipi kijana mbona […]

Read More..

Nisha Alia Tena, Amfungukia Baba Kijacho

Post Image

Staa wa Bongo Movies, Nisha kwa mara nyingine tena ametoa kilio chake kwa mwanaume aliyembebesha ujauzito alionao hivi sasa na kuachana. Nisha ambae hadi sasa ni ‘single parent’ amefunguka kwenye ukurasa wale wa Instagram kuwa atamlea mtoto ajae kama alivyomlea mtoto wake wa kwanza. “Mwanzo nlisema ok nitashinda..but siku baada ya siku najua atahitaji kukujua..kikubwa […]

Read More..

Calisah: Kama Sio Mimi ni Wema Aliyevujisha...

Post Image

Sinema ya model Calisah imezidi kushika kasi – amefunguka kwa kudai kuwa ni yeye au Wema Sepetu ndio waliovujisha video inaowaonesha wakilana denda. Siku chache zilizopita mwanamitindo huyo wa kiume alikamatwa na polisi kwa kosa la kudaiwa kusambaza kipande hicho cha video lakini baadae aliachiwa. Akiongea na kipindi cha Campus Vibes cha Times FM, Calisah […]

Read More..

Raymond Atuhumiwa Kuiba Mistari Kwenye Wimb...

Post Image

Msanii wa WCB, Raymond anatuhumiwa kutumia baadhi ya mistari ya wimbo wa msanii wa muziki wa Singeli, Manyo Lee kwenye wimbo wake mpya wa ‘Sugu’. Akiongea na kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Manyo Lee amesema, “Mimi nilisikia kwa watu tu kuwa dogo kachukuwa mashairi yangu. Juzi kati lilifanyika tamasha kubwa tu nikaona akiimba […]

Read More..

Kigwangalla Akifunga Kiwanda cha Afro-Ameri...

Post Image

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla, ameendelea na usimamizi wa Operesheni Maalum ya kufuatilia na kuufumua mtandao wa Viroba na Pombe feki na haramu nchini. Mchana huu amelazimika ku na vinginevyo ambavyo vimekutwa havina vibali vya TFDA na havina usajili wa TFDA, havina Batch Number ya kutambua […]

Read More..

Picha: EATV Awards Yafanya Semina na Wasani...

Post Image

Tuzo za EATV Awards 2016 Jumatano hii imefanya semina maalumu na wasanii wanaowania tuzo kutoka katika vipengele mbalimbali vya tuzo hizo ambazo kilele chake kinatarajiwa kuwa Desemba 10 mwaka huu. Msanii wa filamu Gabo akiuliza jambo Semina hiyo ilihusisha viongozi wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA), waandaaji wa tuzo hizo (EATV) pamoja na nominees kutoka […]

Read More..

Sina ‘Bifu’ na Bella – Chaz Baba

Post Image

Mkongwe wa muziki wa dance nchini Chaz Baba amesena hana bifu lolote na msanii mwenzake Christian Bella na kwamba yeye ni ‘Team Bella’ damu. Pia Chaz Baba amesema ni wakati tu haujafikia na muda ukifikia watakutana na Bella kwa kuwa tangu Bella anaingia Tanzania alikuwa anamuelewa na sasa anafanya vizuri katika muziki na mashabiki wake ndo mashabiki waliokuwa […]

Read More..