-->

Monthly Archives: May 2017

AliKiba Mwendo Wake wa Kobe Ila Mambo Yake ...

Post Image

Alikiba aka King Kiba ni kati ya wanamuziki wa Africa ambao wanashabikiwa na kuwa na umaarufu wa hali ya juu. Hii yote inatokana na utamu wa sauti aliyojaliwa nayo, na kipaji cha mashairi matamu ambayo kwakweli yamekuwa yakiwaburudisha mashabiki lukuki Duniani. Alikiba ambaye kwasasa yuko chini ya kampuni kubwa ya muziki Duniani Sony Music, anauwezo […]

Read More..

VIDEO:Young Dee: Sijatelekeza Mtoto Wangu

Post Image

Msanii Young Dee a.k.a Pakarasta amesema yeye hawezi kulea mtoto wake na wala hajui ulezi na ndiyo maana mtoto wake amempeleka kwa mama yake ili aweze kupata malezi mazuri na misingi ya kiimani zaidi. Young Dee amebainisha hayo baada ya kuenea kwa taarifa mbalimbali kutoka katika mitandaoni ya kijamii ambazo zilikuwa zikidai msanii huyo amemtelekeza mtoto […]

Read More..

VIDEO: Aliyeliombea gari lisichukuliwe na m...

Post Image

Video moja inayomwonyesha mkazi wa Morogoro Bw. Nyangusi Laiser akiwa anaombea gari lake aina ya Toyota Land Cruiser lisichukuliwe na mafuriko, liligeuka kuwa burudani kwenye mtandao baada ya kusambaa sana kwenye mtandao. Bw Laiser aliandika kwenye ukurasa wake wa Fesibuku siku ya Jumanne, ambapo tukio lilitokea, kwamba alikuwa kwenye gari na mke wake pamoja na […]

Read More..

Jokate: Sasa Nawaza Noti Tu

Post Image

MWANAMITINDO Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’ amefunguka kuwa, misukosuko aliyokumbana nayo kwenye maisha ya kimapenzi imetosha kwani kama ni maumivu ameshayaonja na sasa hakuna anachowaza zaidi ya kujirundikia noti kwa kufanya kazi kwa nguvu. Akizungumza na Akizungumza Ijumaa, Jokate ambaye pia ni Kaimu Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa Umoja wa Vijana wa Chama […]

Read More..

Harmorapa Amjibu Afande Sele

Post Image

Wiki iliyopita Mfalme wa Rhymes nchini Tanzania, Afande Sele alizungumzia hali ya muziki ilivyo kwa sasa na kwenye mazungumzo hayo alisikika akisema hajui ngoma yoyote ya Harmorapa na hata kwa mara ya kwanza kumuona ni pale alipotokea kwenye tukio la Nape kushikiwa Bastola, hivyo haelewi muziki anaoufanya zaidi ya kumuona mitandaoni tuu. Hatimaye Harmorapa amemjibu. […]

Read More..

Hakuna Zaidi Yangu – Chid Benz

Post Image

Rapa Chid Benzi amefunguka na kusema kwa Tanzania hii hakuna msanii mkali kama yeye na hatatokea msanii ambaye anaweza kuchukua nafasi yake kwa mashabiki wake sababu hata hao mashabiki zake wanatambua kuwa hakuna msanii mkali zaidi ya Chuma. Chid Benzi amesema hayo alipokuwa akiwatoa hofu watu juu ya yeye kurudi kwenye muziki na kusema muda […]

Read More..

Mambo 9 Kurudisha Soko la ya Kuzingatia Fil...

Post Image

KUTOKANA na wasanii wa fi lamu za Kibongo kuwa kwenye mikakati mizito ya kuhakikisha soko la kazi zao linarejea kwenye ubora wake kwa madai kuwa filamu za nje zimeua soko la ndani, kuna haja ya kuyazingatia haya yanayochangia kufeli kwao ili kupaa na kufi kia levo ya kimataifa. UBORA WA STORI Ninapozungumzia ubora wa stori […]

Read More..

Chura Ameniunganisha na Watu -Snura

Post Image

Msanii wa muziki Bongo Snura Mushi a.k.a Snura amefurahishwa na mashabiki aliowapata wakati anatoa nyimbo ya chura mwaka jana mwezi wa nne. Snura ameeleza kufurahishwa kwa kuongeza idadi ya mashabiki hao kupitia kipindi cha EIGHT cha TVE kuwa nyimbo yake ya chura ilimuwezesha kupata mashabiki wengi katika soko lake la muziki na anaimani bado anao […]

Read More..

Video: Chid Benz afunguka kwa mara ya kwanz...

Post Image

Rapa Chid Benz amefunguka kwa mara ya kwanza tangia atoke Rehab alikokuwa akipata matibabu ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya na amewaasa vijana watu,iaji wa Tanzania kuacha kabisa mchezo huo. Chid Benz ambaye anaonekana mwenye afya na uso wenye furaha, amesema madawa ya kulevya sio ya kuyazungumzia. Amesema kama mtu hataki kujutia maisha […]

Read More..

Shilole Ashindwa Kufika Mahakamani Kutoa Us...

Post Image

Dar es Salaam. Msanii wa muziki wa kizazi wa Bongo Fleva na filamu, nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole ameshindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi katika kesi ya matumizi mabaya ya mtandao kwa kuwa anaumwa. Leo (Jumatano) Shilole alipaswa kutoa ushahidi katika kesi hiyo inayomkabili mwanafunzi wa Chuo cha Bandari, Thomas Lucas (20) inayosikilizwa mbele ya […]

Read More..

Nilitaka Kujua Lipumba Amepatwa Nini –...

Post Image

Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Dr Josephat Gwajima amefunguka na kusema Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ni rafiki yake hivyo alitaka kuonana naye ili aweze kujua Professa Ibrahim Lipumba anaharibu vipi chama. Mchungaji Gwajima amesema hayo leo alipokutana na waandishi wa habari baada ya kumaliza mazungumzo na […]

Read More..

Prof. Jay Ameanza Kunielewa- Steve Nyerere

Post Image

Mchekeshaji na muigizaji wa bongo ‘movie’ Steve Nyerere amefunguka mengine mapya kwa kudai hana haja tena ya kuendelea kutukanana na watu wasiojielewa kwa kuwa ameshajitokeza mkombozi wake mwenye akili na kutambua kilio chake kinamaana gani. Steve amesema hayo baada ya kile kinachoaminika kuwa Mbunge wa Mikumi, Mhe. Joseph Haule kusimama mbele ya Bunge la Jamhuri […]

Read More..

Diamond Afunguka Haya Baada ya Profesa Jay ...

Post Image

Msanii Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz leo kupitia akaunti yake ya Instagram ameeandika maneno yanayoashiria kutokufurahia hotuba ya mbunge wa Mikumi Joseph Haule a.k.a Prof Jay. Diamond aliandika maeno hayo yanyosomeka “Ndio Maana kwenye Jimbo lako sikuja kupiga kampeni bro…kwakuwa niliijua mapema thamani na umuhimu wa Uwepo wako kwenye hilo jengo….. @professorjaytz Pro .Jay katika […]

Read More..

Baraka Akiri Naj Kumpoteza Kwenye Media

Post Image

MWANAMUZIKI anayefanya vizuri kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Baraka Andrew ‘Baraka The Prince’ hivi karibuni amekiri kuwa, mpenzi wake wa sasa Najma Dattan ‘Naj’ ndiye amesababisha akauke kwenye vyombo vya habari ‘media’. Akichonga na Mikito Nusunusu, Baraka alisema kuwa kipindi cha nyuma kabla hajawa kwenye uhusiano na Naj alikuwa hajatulia hivyo wasichana wengi […]

Read More..

Linah Sanga Afungukia Kuachia Tumbo Wazi

Post Image

Linah Sanga ‘Ndege Mnana’ amefunguka na kuweka wazi kwamba haoni tatizo yeye kupiga picha za kuachia tumbo lake lenye ujauzito wazi kwani picha ni za kawaida sana wala hazina matatizo yoyote. Linnah amefunguka hayo kwenye kamera za eNewz na kudai kwamba hawezi kumfurahisha kila mmoja ndio maana anafanya kile ambacho anahisi kipo sahihi kwa upande wake […]

Read More..

Si Mchina ni Umbo Langu – Sasha

Post Image

MWIGIZAJI chipukizi katika tasnia ya filamu Bongo Sophia Salim ‘Sasha’ mwenye umbo la Kibantu amesema kuwa ni umbile lake na hajui wala hajawahi kutumia dawa za Kichina kama vile ambavyo wengine wanadaiwa kufanya kitu hicho yeye amezaliwa hivyo na anajivunia kuwa hivyo. “Jamani hili ni umbo langu halisi nimeumbwa hivi na sijawahi wala sijui hizo […]

Read More..

Jux Afungukia Picha za Vanessa na Wanaume

Post Image

Msanii Jux ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake ‘Umenikamata’ amefungaka na kusema kitendo cha Vanessa Mdee kuonekana akipiga picha na wasanii mbalimbali au wanaume hakimpi shida kwani yeye anaamini zile ni kazi. Jux anasema yeye aliamua kutoweka wazi mambo yake na Vanessa kutokana na ukweli kwamba ilifika wakati watu walikuwa hawazungumzii kazi zao zaidi […]

Read More..

Masogange Ajisalimisha Kisutu

Post Image

Dar es Salaam. Msanii, Agnes Gerald maarufu kama Masogange (28) amejisalimisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Kabla ya Masogange kujisalimisha mahakama ilitoa hati ya kumkamata baada ya kushindwa kuhudhuria mara mbili kwenye kesi hiyo inayomkabili. Hatua hiyo ya kutaka kukamatwa kwa Masogange ilikuja baada ya upande wa mashtaka kuomba mahakama kutoa hati ya kumkamata […]

Read More..